UJENZI PAMOJA NA HUDUMA ZA USHAURI
WHI imesajiliwa kama Mkandarasi Daraja la 1 na mshauri elekezi wa ujenzi na kupitia Idara ya Uendeshaji imefanikiwa kujenga Ofisi za Serikali na kutoa Ushauri Elekezi kama ifuatavyo:
1. Ofisi ya Rais (UTUMISHI)
WHI inatoa huduma ya ushauri elekezi katika ujenzi wa Jengo la Ofisi ya UTUMISHI eneo la Mtumba Dodoma.
2. Ujenzi wa ukuta kwa nyumba za Chuo Kikuu cha Dodoma
WHI imejenga ukuta kwa nyumba za Chuo Kikuu cha Dodoma.
3. Ujenzi wa Lango Kuu la Chuo Kikuu cha Dodoma
WHI inatoa huduma za ujenzi wa Lango Kuu la Chuo Kikuu cha Dodoma.
4. Ujenzi wa Nyumba za Watumishi – Mkulazi Dakawa
WHI inajenga nyumba za Wafanyakazi wa Kiwanda cha Sukari – Mkulanzi Dakawa
5. Ujenzi wa Maabara ya Ukaguzi na Uchunguzi
WHI imekamilisha ujenzi wa Maabara ya Ukaguzi na Uchunguzi Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Dodoma.
6. Ukarabati Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Mbeya
WHI imefanya ukarabati wa Jengo la Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Mbeya.
7. Ukarabati Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Shinyanga
WHI inafanya Ukarabati Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi Shinyanga.
8. Ukarabati Ofisi ya Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA)
WHI imekamilisha ukarabati wa Ofisi za Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) Jijini Mwanza.
9. Jengo la Mfuko wa Mawasiliano (UCSAF) – Dodoma
WHI imetoa ushauri elekezi katika usimamizi wa Jengo la Makao Makuu ya Mfuko wa Mawasiliano (UCSAF) Jijini Dodoma.
10. CHUO CHA UTUMISHI SINGIDA
WHI imekamilisha Ujenzi wa Jengo la Chuo cha Utumishi Singida.